Rais Samia pia amemteua Katibu Mkuu wa CCM Emmanuel Nchimbi kuwa mgombea mwenza wake katika uchaguzi mkuu utakaofanyika baadae mwaka huu.
Nchimbi ni mwanasiasa mwandamizi na ameshika nafasi mbali mbali ndani ya CCM na serikali yake kwa miongo mitatu iliyopita. Amewahi kushika nafasi ya Waziri wa Mambo ya Ndani katika serikali ya Kikwete na aliteuliwa kuwa balozi na hayati John Pombe Magufuli na kuiwakilisha Tanzania nchini Brazil na baadae Misri.
Kwa mujibu wa Rais Samia, Makamu wa Rais wa sasa Philip Mpango alimuomba apumzike na ameridhia na ndio maana amemteua Nchimbi.
Mpango ataendelea na majukumu yake kama Makamu wa Rais mpaka uchaguzi utakapofanyika, sawia na Nchimbi ambaye ataendelea na majukumu yake ndani ya chama kwa sasa.